KUTOKANA na ndoa hiyo kuwa ya aina yake, hivi karibuni waandishi wetu
walimuweka kati Bob Junior na kumbana kwa maswali ya “why, kwanini,
ikawaje” aoe kimyakimya wakati yeye ndiye ‘prezidaa’ wa masharobaro?
Bob Junior akafunguka: “Nilifunga ndoa Desemba mwaka jana.
Nililazimika kuoa kimyakimya kutokana na masharti ya wazazi wa pande
zote mbili kwamba ndoa isifungwe kwa mbwembwe.”
Alisema, hata idadi
ya wahudhuriaji katika ndoa hiyo ilidhibitiwa, hivyo kuruhusu ndugu na
marafiki wachache kushuhudia tukio hilo.
“Kikubwa ni kufunga ndoa inayompendeza Mungu ili atupe Baraka zake na tuishi katika maisha yanayompendeza.
“Kwa Watanzania, napenda wajue tu ukweli kwamba nimeoa na mke wangu
anatarajiwa kujifungua hivi karibuni,” alisema Bob Junior a.k.a Mr.
Chocolate.
KAULI YA KWANZA YA BOB JUNIOR KUHUSU NDOA ALIYOFUNGA KIMYA KIMYA
Written By Unknown on Saturday, January 12, 2013 | 4:29 AM
Labels:
burudani
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !